Sunday, March 25, 2018

MAMBO YA MUHIMU KUZINGATIA UNAPOBUNI NA KUJENGA NYUMBA



1.MLANGO MKUBWA WA KUINGIA NDANI(MAIN DOOR)
picha kwa hisani ya Pongu J

Mlango mkuu wa kuingia kwenye nyumba ndio unaokaribisha anayeingia ndani.Kiimani ni lango la kukaribisha nguvu zote zenye faida na zenye madhara.Pia ni mlango mkuu wa kutoka ndani ya nyumba.
·         Ni muhimu mlango wa kuingia ndani uoane ama uwe katika uelekeo mmoja na lango kuu la kuingia (Gate)

·         Lango kuu(gate)  na mlango wa kuingia ndani ni vema view upande mmoja. Sababu kubwa ni kufanya kuwa na urahisi kuingia lango kuu na kutembea moja kwa moja kwenda kwenye mlango wa nyumba pasipo kuzinguka.Pia ni rahisi kujua anayeingia na kutoka
·         Mlango mkuu wa kuingia ni muhimu uwe mkubwa na iwe miwili(double door) yaani ufunguke sehemu mbili.

Pia ni muhimu nyumba kuwa na milango miwili ya nje kuruhusu kuingia na kutoka kwa urahisi pale inapohitajika, na kufanya hewa kuingia na kutoka na kuufanya mzunguko wa hewa ndani ya nyumba

·         Upande wa kuingia unapaswa kuwa mkubwa kuliko wa kutoka.Sababu kubwa ni kwamba,hapa ndipo hewa(air) inavuma kutoka nje kwenda ndani.Unapaswa iignie kwa wingi na kutoka kidogo kufanya nyumba ipumue(hewa izingike vema kwenye nafasi zote
·         Mlango wa kuingia unapaswa kuwa mkubwa kuliko yote kwenye nyumba.Sababu kubwa ni kuruhusu vitu kuingia na kutoka kama samani na vifaa vingine vikubwaPia nguvu huingia kupitia hapa,hivyo ni muhimu kuingia kwa wingi.

·         Ni muhimu mlango huu wa kuingia ufungukie ndani na kwa mzunguko wa akrabu (clockwise).Sababu kubwa ni kwamba inasaidia kuingia kwa urahisi kwa kusukuma.Pia ni rahisi ukiwa ndani unafungua kwa kutumia mkono wa kushoto na kuwa rahisi kukaribisha ama kuwa tayari kupokea kwa mkono wa kulia.

·         Mlango mkuu unapaswa kuwa na kizingiti.Epuka kuweka viatu mbele ya mlango wa kuingia ndani ya nyumba,sababu ni kuzuia wadudu na wanyama kuingia. Viatu huweza kuvuta wadudu kama nzi, na huweza kusababisha kujikwaa.Pia huleta picha mbaya mbele ya nyumba
·         Mlango mkuu ni muhimu uwe juu kutoka usawa wa ardhi, na kuufikia panapaswa kuwa na ngazi chache kuufikia na zinapaswa kuwa na idadi ya namba witiri. Sababu ya msingi ni kuzuia maji na wanyama wanaotambaa kufikia kirahisi.Pia kuwa juu kutoka usawa wa ardhi kunasababisha taka kutoingia ndani.

Sababu kwa nini ni muhimu kuwa na ngazi chache ambazo idadi yake ni witiri ni kwa sababu watu wengi hutumia mkono wa kulia,huanza kupanda ngazi kwa kunyanya kwanza mguu wa kulia,hivyo anapopanda atamaliza kwa kufika na mguu wa kulia.

·         Mlango mkuu unapaswa kuonekana kwa urahisi na uvutie.Sababu ni kwamba mgeni anapofika anapaswa kuuona kwa urahisi na umvutie(usiwe gizani na usiwe mweusi)
·         Mlango uwe unavutia na ubunifu wa kutosha ikiwemo picha ama alama zenye kuvutia.Bianadamu hupenda kuona vitu vyenye kuvutia

·         Mlango unapaswa utengenezwe zaidi kwa kutumia mbao kwa sababu mbao hudumu nan i rahisi kuweka nakshi na urembo

**ZINGATIA-Mbao inayotumika kutengeneza mlango isitokane na miti isiyokomaa,sitokane na miti inayotoa maua mazuri ya biashara wala harufu kali na isitokane na miti ambayo ipo hatarini kutoweka ili kuzuia upotevu wa miti yenye faida zaidi kwa matunda,maua na yenye historia.
Picha kwa hisani ya mtandao



JE NI MAMBO GANI UNAPASWA KUYAEPUKA UNAPOBUNI MLANGO MKUBWA WA KUINGIA NDANI (AMA KUJENGA)
1.       Kwa nyumba za kuishi epuka mlango wenye kuzunguka (circular door) nay a kutembea (sliding door) kwa sababu kubwa ni kwamba haitoi urahisi katika kutumia na haidumu

2.       Epuka mlango wako mkubwa kuingia kwenye nyumba kutazamana moja kwa moja na mlango mkuu wa nyumba nyingine.Pia mlango usitazamane na msikiti,kanisa ama mahakama. Unapofungua mlango wa nyumba yako mtu huweza kutazama moja kwa moja ndani

3.       Epuka kuwa na miti mikubwa ama kitu kisichohamishika mbele ya mlango wako,utakuzuia kuonavitu vilivyo mbele ya mlango na kisaikolojia  usababisha pingamizi ama vizuizi.

4.       Epuka mlango kutazama moja kwa moja gofu/magofu,unapofungua asubuhi utatazama gofu

5.       Epuka kujenga tanki chini(underground tank) ama tanki la maji taka mbele ya mlango wa kuingia.iwapo itahitajika kusafisha ama kufanya marekebisho itasumbua kupita

6.       Epuka kuweka mlango wa kuingia ndanin ya nyumba kwenye kona ya nyumba.Ni vigumu kupangilia samani kwa sababu kona itatumika kwa ajili ya nafasi ya kutembea.

7.       Epuka kuwa na ukuta unapofungua tu mlango wa kuingia, hewa na mwanga utazuiliwa kupita

8.       Epuka mlango unaojifunga wenyewe. Endapo patakuwa na upepo mkubwa mlango unaweza kujifunga huku funguo zikiwa ndani.

9.       Epuka mlango uliochakaa na unaotoa kelele unapofunguliwa/kufungwa-unaonesha udhaifu wa mlango, uzembe

Je, makala hii imekusaidia kwa njia yoyote? Kama ndio usisite kuwashirikisha wengine kusoma waelimike.
Kwa maswali kuhusu ujenzi usisite kuwasiliana nami
PONGU J- +255 765046644

No comments: