Sunday, July 19, 2015

KUKAMILISHA NDOTO YA NYUMBA YAKO

Picha ikionesha sehemu za ndani za nyumba kadiri ya muono wa msanifu-Imesanifiwa na P.J



Kila mtu anapotaka kujenga nyumba,huwa na picha ya nyumba aliyenayo.
Uzoefu wangu unaonesha kwamba watanzania wengi huwa hawana muono wa kitu wanachokitaka.Ukikutana na watu wengi wanaohitaji ramani ,huishia kufananisha maono yao na nyumba aliyeiona kwa nje,eitha ya jirani ama rafiki ama mtu maarufu.


Kwa kifupi ningepnda tushirikishane ujuzi kidogo.Ili kuitafsiri ndoto kuhusu kitu unachokitaka ni vizuri kutazama yafuatayo


1.Ukubwa-ukijumuisha,urefu,upana,ukubwa wa vyumba,idadi ya watu watakaotuia nyumba


2.Uhusiano kati ya nafasi moja na nyingine,ni vema picha ulionayo katika fikra zako iwe na tafsiri /picha ya jinsi sehemu moja na nyingine zinavyooana-mfano sebule na dining na vyumba n.k


3. Iwe na picha ya rangi utakazopiga ktka nyumba,kama ni rangi moja ijulikane,kama ni rangi tofauti ijulikane,kama ni aina ya texture ijulikane.Rangi pia ijumlishe ndani,nje,paa


4.Ndoto ni lazima iwe na picha ya jinsi madirisha,milango na vitu vingine vitakavyokuwa.Hii inajumuisha aina ya malighafi itakayotumika,rangi/texturena ukubwa

5.Ni vema ndoto ikawa na picha ya mazingira yanayokuzunguka.Kitu ukiwazacho moyoni mwako huwa.Jinsi unavyofikiri ndivyo unavyokuwa na mazingira huwa vile unavyoyatengeneza.Hivyo kabla ya kuanza kuamua kujenga ni muhimu ukawa na picha ya jinsi mazingira yatakayokuzunguka yatakavyokuwa.Utapaswa kujua bustani inayozunguka,maua,miti ,uoto wake kwa ujumla,majirani


6.Mwisho kabisa tafsiri ya ndoto yako iende kwenye gharama unayotaka kuitumia

Picha kwa hisani ya Pongu J

Nawasilisha na nakaribisha maoni.

No comments: