Wednesday, July 8, 2015

UCHAGUZI WA RANGI KATIKA NYUMBA

Rangi katika nyumba ina faida kuu mbili,zikiwa ni kuongeza nakshi (kupendezesha ) na kazi ya pili ni kulinda kuta.

unaionaje rangi hii






picha zote ni mali ya Joseph P.

Rangi za kuta zinaweza kuwekwa katika makundi mawili ya rangi msingi na rangi sekondari (upili)
Rangi msingi ni rangi ambazo hupigwa ili kuwezesha rangi upili kudumu.Hujulikana kama primer kwa lugha ya kiingereza

Makala hii fupi inalenga kushirikisha wasomaji na wale ambao wangependa kujenga kuhusu uchaguzi wa rangi.

Ni wazi kuwa kila mtu ana uchaguzi wake wa rangi,na mara nyingi kuvutia kwa rangi ni baina ya mtazamaji na maono yake.

Zipo rangi zilizopoa na zinazong'aa sana.Ni sawa na kusema rangi zinazoakisi zaidi mwanga na zile za kutunza mwanga.

Ndugu msomaji ,nini maoni yako kuhusu rangi za kung'aa na rangi za kupoa.Je wewe binafsi unapenda nyumba yako iweje ukijenga.Kuanzia rangi ya paa mbaka kuta.Unapata picha gani unapofikiri kuhusu nyumba yako?

Niambie wewe umependa rangi ipi kati ya hizo juu.Una maoni gani kwa msanifu wa nyumba hizo hapo juu kuhusu rangi?
Tujadiliane

No comments: