Monday, March 26, 2018

KWA NINI NI MUHIMU KUZINGATIA PANDE ZA DUNIA UNAPOCHAGUA SEHEMU YA KUJENGA NA KUJENGA?




Kulingana na mapokeo na  utaalamu toka kale, ni muhimu sana kuzingatia pande za dunia unapotaka kujenga,hasa unapochagua sehemu ya kujenga.

Fuatana nami kupitia makala hii uelimike kuhusu uchaguzi wa eneo la kujenga
Picha ikionesha pande za dunia






UELEKEO WA KIWANJA (SITE ORIENTATION)

Uelekeo wa kiwanja maana yake ni mahali(nafasi) kilipo kiwanja kwa kuzingatia dira. Hutanabaishwa kwa kutazama upande wa mbele ya kiwanja chako unapotazama.Unaposimsms kwenye kiwanja chako na kutazama ilipo barabara, upande unaoutazama ndio uelekeo wa kiwanja chako.Kama kiwanja kina barabara upande wa kaskazini, basi uelekeo wako ni kaskazini(North facing site)

Kutokana na mapokeo  zipo pande nane ambazo huzingatiwa kulingana na lilipo jua.Pande hizi hutokana na pande nne kuu ambazo ni

  • Mashariki-Unatambulika ni upande ambao jua huchomoza

  • Magharibi-Unatambulika kuwa ni upande jua linapozama

  • Kaskazini-Unatazama mashariki,upande ulio kushoto kwako ni Kaskazini

  • Kusini-Utazamapo mashariki,upande uliopo kulia kwako ni kusini

Kona ambazo pande mbili kati ya pande kuu nne zilizotajwa hukutana,ni muhimu kwa sababu kani ya mvutano toka pande kuu nne huungana.

  • Kaskazini mashariki-Ni upande ambao pande mbili za kaskazini na mashariki zinakutana Kaskazini Magharibi-Ni upande ambao pande mbili za kaskazini na magharibi zinakutana

  • Kusini Magharibi-Ni upande ambao pande mbili za kusini na magharibi zinakutana

  • Kusini Mashariki-Ni upande ambao pande mbili za kusini na mashariki zinakutana




KWA NINI MWELEKEO WA KIWANJA NI MUHIMU SANA WAKATI WA KUCHAGUA KIWANJA CHAKO?

Jua ni muhimu sana katika maisha ya viumbe hai.
Jua husababisha mimea kujitengenezea chakula chake,ambayo baadae wanadamu hula.Jua husaidia mwili wa binadamu kutengeneza Vitamini D.Jua pia huleta nuru.Kwa kifupi ni vigumu kutofautisha jua na uhai wa viumbe.Ukiachilia mbali faida za jua,pia zipo hasara kwa viumbe,akiwwemo binadamu

Hivyo ni muhimu wakati  wa kupangilia nyumba, ni muhimu kuhakikisha binadamu anahakikishiwa miale ya jua yenye faida na kukingwa na miele mikali ya jua yenye madhara.Vymba na nafasi zote zinazohitajika kwenye nyumba ni lazima zipangiliwe kuhakikisha zinapata mwanga wa jua wenye faida na kukingwa na miale yenye kuleta athari
Mwelekeo wa nyumba yako kuzingatia mawio na machweo ya jua ni muhimu


JE NI UPANDE UPI MZURI KWA KIWANJA CHAKO?

Pande zote zinafaa,zikiwa zina faida na hasara yake.Mpangilio wa mji huzingatia uwepo wa barabara katika pande zote za mtaa(Kwa maeneo yaliyopangiliwa tu) na pande zote huhitajika kuwepo majengo(nyumba) ili kufanya mtaa(mji) uvutie na kufikika kwa urahisi

KIWANJA KINACHOTAZAMA MASHARIKI

Upande huu ndipo jua linapochomoza.Miale yenye faida huwa jua linapochomoza.Utafiti unaonesha jua la majira ya saa nne(asubuhi) husaidia mwili kuzalisha vitamin D.Hivyo kiwanja kitazamacho upande huu hutoa nafasi nzuri zaidi kupangilia nafasi zako katika nyumba,hasa ikitazama upande huu. Ukiamka unakutana na mwanga wa jua unaochochea ubongo kufanya kazi vema.Katika baadhi ya tamaduni upande huu huhusishwa na ucha Mungu, uaminifu, elimu na ibada.

UPANDE WA KASKAZINI

Upande huu una uhusiano mzuri na kuvuma kwa upepo na miale ya jua.Katika imani mbalimbali kiwanja kitazamacho Kaskazini huhusiana na nguvu na utawala

UPANDE WA KUSINI

Mara nyingi viwanja vyeye kutazama upande huu havipendelewi sana kwa sababu huhitaji zaidi umakini katika kupangilia nyumba yako na mazingira yanayohusiana na nyumba yako.Viwanja hivi hufaa zaidi kwa matumizi ya biashara kuliko ya makazi.

UPANDE WA MAGHARIBI

Ni upande jua linapozama.        

Ni muhimu kuwa makini unapopangilia nyumba yako kwa kiwanja kitazamacho upande huu

Je Makala hii imekusaidia kujifunza chochote?Kama ndio washirikishe wengine waelimike.
Usisite kuniandikia maoni yako na maswali kuhusu ujenzi.

Sunday, March 25, 2018

NYUMBA YA VYUMBA VITATU VIKUBWA

Hii ni nyumba ya vyumba 3,iliyosanifiwa kwa kuzingatia wale wanaopenda vyumba vikubwa kiasi na wenye eneo la kutosha kujenga na kuifurahia mandhari inayozunguka nyumba

Unaweza kujenga nyumba hii kwenye kiwanja chenye ukubwa kuanzia meta 18 kwa 25.

Mvuto wake na mpangilio  ndani na nje utakufanya ufurahie kuishi na kuiita nyumbani



NYUMBA YA VYUMBA 3

Hii ni nyumba ya vyumba vitatu ambayo inajumuisha sebule,chumba cha chakula(dining), jiko lenye stoo ,common toilet na chumba kimoja kati ya hivyo vitatu ni self contained.
Unaweza kuijenga kwenye kiwanja cha meta 15 kwa meta 20 na kupata nafasi ya kuegesha gari,kucheza watoto,kupumzika na shughuli nyingine muhimu


mwonekano wa upande mmoja,nyuma ya nyumba

mwonekano wa mbele
Je,ni nini imekuvutia kwenye nyumba hii?Niandikie maoni yako,
Wasilisha Email: nyumbaboratz@gmail.com

MAMBO YA MUHIMU KUZINGATIA UNAPOBUNI NA KUJENGA NYUMBA



1.MLANGO MKUBWA WA KUINGIA NDANI(MAIN DOOR)
picha kwa hisani ya Pongu J

Mlango mkuu wa kuingia kwenye nyumba ndio unaokaribisha anayeingia ndani.Kiimani ni lango la kukaribisha nguvu zote zenye faida na zenye madhara.Pia ni mlango mkuu wa kutoka ndani ya nyumba.
·         Ni muhimu mlango wa kuingia ndani uoane ama uwe katika uelekeo mmoja na lango kuu la kuingia (Gate)

·         Lango kuu(gate)  na mlango wa kuingia ndani ni vema view upande mmoja. Sababu kubwa ni kufanya kuwa na urahisi kuingia lango kuu na kutembea moja kwa moja kwenda kwenye mlango wa nyumba pasipo kuzinguka.Pia ni rahisi kujua anayeingia na kutoka
·         Mlango mkuu wa kuingia ni muhimu uwe mkubwa na iwe miwili(double door) yaani ufunguke sehemu mbili.

Pia ni muhimu nyumba kuwa na milango miwili ya nje kuruhusu kuingia na kutoka kwa urahisi pale inapohitajika, na kufanya hewa kuingia na kutoka na kuufanya mzunguko wa hewa ndani ya nyumba

·         Upande wa kuingia unapaswa kuwa mkubwa kuliko wa kutoka.Sababu kubwa ni kwamba,hapa ndipo hewa(air) inavuma kutoka nje kwenda ndani.Unapaswa iignie kwa wingi na kutoka kidogo kufanya nyumba ipumue(hewa izingike vema kwenye nafasi zote
·         Mlango wa kuingia unapaswa kuwa mkubwa kuliko yote kwenye nyumba.Sababu kubwa ni kuruhusu vitu kuingia na kutoka kama samani na vifaa vingine vikubwaPia nguvu huingia kupitia hapa,hivyo ni muhimu kuingia kwa wingi.

·         Ni muhimu mlango huu wa kuingia ufungukie ndani na kwa mzunguko wa akrabu (clockwise).Sababu kubwa ni kwamba inasaidia kuingia kwa urahisi kwa kusukuma.Pia ni rahisi ukiwa ndani unafungua kwa kutumia mkono wa kushoto na kuwa rahisi kukaribisha ama kuwa tayari kupokea kwa mkono wa kulia.

·         Mlango mkuu unapaswa kuwa na kizingiti.Epuka kuweka viatu mbele ya mlango wa kuingia ndani ya nyumba,sababu ni kuzuia wadudu na wanyama kuingia. Viatu huweza kuvuta wadudu kama nzi, na huweza kusababisha kujikwaa.Pia huleta picha mbaya mbele ya nyumba
·         Mlango mkuu ni muhimu uwe juu kutoka usawa wa ardhi, na kuufikia panapaswa kuwa na ngazi chache kuufikia na zinapaswa kuwa na idadi ya namba witiri. Sababu ya msingi ni kuzuia maji na wanyama wanaotambaa kufikia kirahisi.Pia kuwa juu kutoka usawa wa ardhi kunasababisha taka kutoingia ndani.

Sababu kwa nini ni muhimu kuwa na ngazi chache ambazo idadi yake ni witiri ni kwa sababu watu wengi hutumia mkono wa kulia,huanza kupanda ngazi kwa kunyanya kwanza mguu wa kulia,hivyo anapopanda atamaliza kwa kufika na mguu wa kulia.

·         Mlango mkuu unapaswa kuonekana kwa urahisi na uvutie.Sababu ni kwamba mgeni anapofika anapaswa kuuona kwa urahisi na umvutie(usiwe gizani na usiwe mweusi)
·         Mlango uwe unavutia na ubunifu wa kutosha ikiwemo picha ama alama zenye kuvutia.Bianadamu hupenda kuona vitu vyenye kuvutia

·         Mlango unapaswa utengenezwe zaidi kwa kutumia mbao kwa sababu mbao hudumu nan i rahisi kuweka nakshi na urembo

**ZINGATIA-Mbao inayotumika kutengeneza mlango isitokane na miti isiyokomaa,sitokane na miti inayotoa maua mazuri ya biashara wala harufu kali na isitokane na miti ambayo ipo hatarini kutoweka ili kuzuia upotevu wa miti yenye faida zaidi kwa matunda,maua na yenye historia.
Picha kwa hisani ya mtandao



JE NI MAMBO GANI UNAPASWA KUYAEPUKA UNAPOBUNI MLANGO MKUBWA WA KUINGIA NDANI (AMA KUJENGA)
1.       Kwa nyumba za kuishi epuka mlango wenye kuzunguka (circular door) nay a kutembea (sliding door) kwa sababu kubwa ni kwamba haitoi urahisi katika kutumia na haidumu

2.       Epuka mlango wako mkubwa kuingia kwenye nyumba kutazamana moja kwa moja na mlango mkuu wa nyumba nyingine.Pia mlango usitazamane na msikiti,kanisa ama mahakama. Unapofungua mlango wa nyumba yako mtu huweza kutazama moja kwa moja ndani

3.       Epuka kuwa na miti mikubwa ama kitu kisichohamishika mbele ya mlango wako,utakuzuia kuonavitu vilivyo mbele ya mlango na kisaikolojia  usababisha pingamizi ama vizuizi.

4.       Epuka mlango kutazama moja kwa moja gofu/magofu,unapofungua asubuhi utatazama gofu

5.       Epuka kujenga tanki chini(underground tank) ama tanki la maji taka mbele ya mlango wa kuingia.iwapo itahitajika kusafisha ama kufanya marekebisho itasumbua kupita

6.       Epuka kuweka mlango wa kuingia ndanin ya nyumba kwenye kona ya nyumba.Ni vigumu kupangilia samani kwa sababu kona itatumika kwa ajili ya nafasi ya kutembea.

7.       Epuka kuwa na ukuta unapofungua tu mlango wa kuingia, hewa na mwanga utazuiliwa kupita

8.       Epuka mlango unaojifunga wenyewe. Endapo patakuwa na upepo mkubwa mlango unaweza kujifunga huku funguo zikiwa ndani.

9.       Epuka mlango uliochakaa na unaotoa kelele unapofunguliwa/kufungwa-unaonesha udhaifu wa mlango, uzembe

Je, makala hii imekusaidia kwa njia yoyote? Kama ndio usisite kuwashirikisha wengine kusoma waelimike.
Kwa maswali kuhusu ujenzi usisite kuwasiliana nami
PONGU J- +255 765046644

Sunday, March 11, 2018

DONDOO MUHIMU KATIKA UCHAGUZI WA KIWANJA CHA KUJENGA NYUMBA YAKO YA KUISHI



Kutafuta kiwanja ni hatua ya awali kabisa kuelekea kujenga nyumba ya ndoto yako. Hatua hii ni muhimu sana kwani ardhi ni gharama na ukishajenga, kubadili maamuzi huleta gharama kubwa zaidi.
Fuatana nami katika makala hii ili uweze kufuhamu ni mambo gani muhimu katika uchaguzi wa kiwanja kwa ajili ya kujenga nyumba ya makazi.
Kwa kifupi, nyumba ya kuishi inapaswa kuwa ni sehemu yenye utulivu , amani, uoto mzuri na ijengwe  sehemu yenye urahisi wa upatikanaji wa huduma muhimu kama maji,usafiri na yenye kuleta msawazo wa mawazo. Pia kila binadamu hupenda amani  ,hivyo ni muhimu uchaguzi wa kiwanja uzingatie dhana hii.
Yafuatayo ni mambo ya msingi unayopaswa kutilia mkazo unapochagua eneo la kujenga




1.      Imani yako kwanza ni muhimu. Inashauriwa usimame kwenye eneo unalotaka kununua ksha sikiliza mvuto wa eneo hilo.Kama panakuvutia moyo wako utakuvutiwa nalo,kama hapana,utakuwa na mashaka nalo



2.      Chunguza historia ya eneo unalotaka kununua.
Unashauriwa kununua eneo lenye historia njema kwa jamii iliyopita kabla yako.Iwe ni sehemu ambayo watu walioishi walikuwa na furaha ,amani na umoja.Sababu kubwa ya kuchunguza ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana wa kimaendeleo kati ya watu walioishi awali na namna ardhi ilivyotumika.Kuishi sehemu yenye watu wenye amani,upendo na mshikamano kutakufanya wewe na kizazi chako uishi pia kwa amani ,upendo na mshikamano.
3.      Kiwanja ambacho kinafikika.
Kiwanja chenye barabara pande zote huhusiana na furaha, afya njema na mafanikio. Huwa na hewa, mwanga na nafasi ya kutosha
Kwa kiwanja kisichokuwa na barabara pande zote,ni muhimu kiwe na barabara kwa upande wa kaskazini ama Mashariki mwake.Sababu ya msingi ni ni kwamba nyumba itakayojengwa itakuwa na mwanga na hewa ya kutosha kuanzia asubuhi.
Katika sehemu za Asia hasa India,kiwanja chenye maji upande wa kaskazini ama mashariki hupendelewa zaidi,sababu ikiwa ni uwezekano mkubwa wa kuwepo mwanga,hewa na mandhari ya kutosha na kwamba miale ya jua ya asubuhi(Ultraviolet light ) husaidia kuua vijidudu kwenye maji na kuyafanya yafae kutumika
4.      Hakikisha eneo unalonunua ni la makazi ama makazi na biashara.
Itakufanya uepuke na usumbuufu kubomolewa ama kuwa na hofu ya kuhamishwa.Hakikisha unafuata taratibu zilizowekwa katika kumiliki ardhi.
Nyumba iliyozungukwa na maji upanse wa mashariki.Picha kwa msaada wa architectureideas.com

Je ni kiwanja cha namna gani hakikufai katika ujenzi wa makazi?
1.      Epuka kiwanja kinachouzwa na mtu aliyepatwa na dhiki/filisika
Kiwanja cha namna hii ni muhimu kinunuliwe kwa uangalifu mkubwa kwa kuzingatia kumwinua mwenye dhiki ama shida.
Ununuzi wa kiwanja cha namna hii kwa malengo ya kujinufaisha wewe zaidi kitakufanya baadae ukose furaha na amani na labda manung’uniko yatokanayo na muuzaji ama jamii inayozunguka yanaweza kukuondolea heshima na utu.
2.      Epuka kiwanja kilicho jirani/kinachopakana  na maeneo ya mikusanyiko mikubwa ya kijamii.
Maeneo haya ni kama kumbi za starehe, kanisa, msikiti , kiwanda, chuo, jeshini,  shule, soko, sehemu stesheni za magari.
Maeneo haya huwa na kelele nyingi  na mara nyingi matumizi ya maeneo haya huadhiri maeneo yaliyo jirani,ikiwemo kubadilishwa kwa matumizi wakati wowote.Ni vigumu kulea watoto na kuwakuza kimaadili katika maeneo yaliyojirani na sehemu nilizozitaja hapo juu.

3.      Epuka kununua eneo linalomilikiwa ama lililomilikiwa na taasisi za kiimani.
Wengi wanaweza wasielewe hili. Wakati wowote taasisi za kiimani huweza kuuza maeneo kwani  ni haki yao ya msingi. Lakini kadiri mahitaji yanapoongezeka miaka kwa miaka,uwezekano mkubwa wa kulihitaji eneo lao la awali hujitokeza.Kwa sababu ni vigumu kushindana na taasisi, ni ukweli usiopingika kwamba mazingira yatakufanya ulazimike kuondoka na kuanza maisha upya,licha ya kwamba utalipwa.
4.      Epuka eneo lililo jirani na sehemu za taka na zenye harufu kali.
Kiwanja chako hakipaswi kuwa jirani na machinjio, mashimo ya taka ngumu na maji taka, mitaro mikubwa ya maji, sehemu wanapotengeneza na kuuza viatu, tairi kwa wingi.
Meneo haya kwa wakati wote yanaweza yakawa na harufu kali na kufanya usiishi kwa furaha na amani.
5.      Epuka kununua kiwanja eneo lenye magofu mengi.
Zipo sehemu ambazo zina magofu mengi yatokanayo na sababu mbalimbali.Mara nyingi maeneo haya huwa ni kivutio cha vibaka, majambazi na wanyama wakali. Kuishi maeno haya huzua hofu.
eneo lenye magofu(picha kwa msaada wa mtandao)

6.      Epuka kiwanja kilichopo eneo lenye dungusi (kakati) (jamii ya mimea kama mpungate.
Sababu ya msingi ni kwamba maeneo yenye mimea hii huwa na udongo dhaifi usio rafiki kwa msingi wa nyumba yako.
7.      Epuka kiwanja  kilicho sehemu yenye mchwa na kumbikumbi wengi
Sababu kubwa ni kwamba ni vigumu kuyaondoa makazi ya mchwa. Mchwa huharibu mbao na hata kudhoofisha msingi na kuta za nyumba. Pia huweza kushambulia samani mbalimbali.
8.      Epuka kiwanja kidogo kilichozungukwa na viwanja vikubwa.
Sababu kubwa ni kwamba mmiliki wa kiwanja kidogo hulazimika kujenga nyumba ndogo ,na wamiliki wa viwanja vikubwa  hujenga nyumba kubwa na kuwa na matumizi mengi zaidi kwenye eneo moja, hivyo mmiliki wa nyumba ndogo (kiwanja kidogo)  hushawishika kujitazama kama mnyonge na mara nyingi hudhani anaonewa(inferiority complex)
9.      Epuka kiwanja chenye mapingamizi ya milima,mabonde na majengo marefu hasa upande wa mashariki na kaskazini mwa kiwanja.
Sababu  kubwa ni kwamba  majengo marefu na milima/mabonde huzuia hewa ya kutosha ,mwanga na huweka kivuli (giza) kwenye nyumba.
Habari njema ni kuwa kiwanja kilicho na milima ama majengo marefu upande wa kusini na upande wa magharibi husaidia kuzuia miale mikali ya mwanga.
10.  Epuka kiwanja kilicho na  nguzo kubwa za umeme kwenye kona ya kaskazini-mashariki.
Sababu kubwa ni kwamba umeme unaopita kwenye nguzo huwa na mawimbi (electrical waves) ambazo huwa na madhara na ukubwa wa nguzo huzuia mwanga na hewa kufikia nyumba itakayojengwa.
11.  Epuka kiwanja chenye nyufa/mipasuko(cracks) na udongo wenye mfinyanzi.
Nyufa kwenye ardhi huwa na uhusiano mkubwa na udongo wa mfinyanzi unaoruhusu maji mengi kutuama.Udongo huu si rafiki kwenye ujenzi na huhitaji gharama kubwa kujenga msingi.

12.  .Epuka kiwanja chenye miti mingi yenye mizizi mirefu na minene
Kama kiwanja unachotaka kujenga  ni kidogo na kina miti mingi yenye mizizi mikubwa na minene inayotambaa,si vema kukinunua kwa sababu mzizi hukua na kusababisha nyufa kwenye msingi na hata kufikia kuta za nyumba
13.  Epuka kiwanja kilichopo kwenye makutano ya barabara kuu hasa makutano yenye kutengeneza herufi T ama Y.
Kiwanja kilichopo kwenye makutano huwa na kelele nyingi, vumbi na wakati Fulani huondoa sitiri(privacy). Makutano yenye kutengeneza herufi T ama Y  kuielekea nyumba (kiwanja) ni rahisi kutokea ajali hasa kwa magari kugongana, watu kugongwa wakati wa kuvuka na pia heleta hofu ya kudhani gari zitagonga nyumba.
nyumba iliyojengwa kwenye kiwanja kilicho kwenye makutano ya barabara


14.  Epuka kiwanja chenye umbo la duara,sambusa ama pembetatu.
Kiwanja cha namna hii kama si kikubwa huongeza ugumu katika kuongeza matumizi na kujenga nyumba yenye ukubwa wa kutosha.Katika imani Fulani viwanja vyenye umbile la duara na pembetatu huhusianishwa na huzuni, umasikini na magonjwa.


Ahsante.
Makala imeandaliwa na Pongu J
+255 717 903089, +255 765046644